Saturday, November 12, 2011

UJUMBE WA WAFANAYABIASHARA KUTOKA SINGAPORE WAWASILI ZANZIBAR LEO


Na Idara ya Habari Maelezo - Zanzibar

Ujumbe wa Wafanayabiashara kutoka Singapore ukiongozwa na Waziri wa Biashara na Viwanda wa nchi hiyo umewasili Zanzibar leo asubuhi kwa ziara ya siku moja.

Kwenye Uwanja wa ndege wakimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar ujumbe huo ulipokelewa na Naibu Waziri wa Biashara ,Viwanda na Masoko Zanzibar Thuweiba Kisaasi , Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Viwanda na Wakulima Zanzibar Mbarouk Omar pamoja na maofisa mbali mbali katika Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar.

Kwa mujibu wa Ratiba iliotolewa na Wizara ya Biashara ,Viwanda na Masoko Zanzibar , Ujumbe huo mchana huu utakuwa na mazungumzo na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd huko
Ofisini kwake Vuga.

Usiku Kwenye Hoteli ya Serena iliopo Mjini Zanzibar Waziri wa Biashara na Viwanda wa Singapore ataelezea juu ya hali ya Biashara nchini mwao na baadae kutatolewa maelezo juu ya nafasi za Vitega Uchumi viliopo Hapa Zanzibar.

Aidha Kamisheni ya Utalii Zanzibar nayo itapata nafasi kuelezea juu ya nafasi ziliopo Zanzibar katika mambo ya utalii na baadae kuwa na Chakula cha Usiku pamoja na kuwa na mazungumzo na Wafanya biashara wa Zanzibar na Wanasiasa.

Ujumbe huo Wawafanyabiashara kutoka Singapore ukiongozwa naWaziri wa Biashara na Viwanda unatarajiwa kuondoka Zanzibar hapo kesho asubuhi.
Kindly Bookmark this Post using your favorite Bookmarking service:
Technorati Digg This Stumble Stumble Facebook Twitter
YOUR ADSENSE CODE GOES HERE

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Labels

 

Pages

Popular Posts

BBC Xclusives

| BongoXclusive © 2009. All Rights Reserved | Sponsored by: Website Templates | Premium Wordpress Themes | consumer products. Thanks to blogger template
Template Style by My Blogger Tricks .com | Back To Top |